Slider[Style1]

HABARI

BONGO MOVIES

BONGO FLEVA

.

BONGO VIDEOS

Style5[ImagesOnly]

STORY ZA INSTAGRAM

JAJA,MSUVA KUNG'AA KWENYE MECHI YA NGAO YA JAMII UWANJA WA TAIFA LEO

Jaja aliingia ‘mzima mzima’ pembezoni mwa lango la Thika kuhakikisha anaiunganishia nyavuni krosi ya Msuva kwa vyovyote na akafanikiwa akimuacha kipa Mganda, Hamza Muwonge anaokota mpira nyavuni. Kwa furaha ya bao hilo, Jaja ambaye alikuwa akizomewa na mashabiki wa Simba SC kila alipokosea alitoka nje ya Uwanja kushangilia bao hilo, kwa shangwe za aina zote alizoweza. Yanga SC haikucheza vizuri kipindi cha kwanza na zaidi ilitegemea kupitisha mashambulizi yake pembeni walipokuwa wakiteleza kwa awamu Simon Msuva, Haruna Niyonzima na Andrey Coutinho. Coutinho alikaribia kufunga mara mbili kwa mipira ya adhabu aliyopiga kutoka nje kidogo ya eneo la penalti, wakati Jaja hakuwa na madhara kabisa kipindi cha kwanza. Nafasi nzuri zaidi kwa Thika ilikuwa dakika ya 20 wakati shuti la Moses Odhiambo lilipodakwa na kipa Deo Munishi ‘Dida’- zaidi ya hapo, safu ya ulinzi ya Yanga SC leo ilicheza vizuri. Kipindi cha pili, kocha Mbrazil Marcio Maximo alianza na mabadiliko katika safu ya kiungo akimpumzisha Hassan Dilunga na kumuingiza Hamisi Thabit, ambaye alikwenda kuibadilisha timu.
 
 
Simon Msuva 
 Mchezaji jaja kutoka kwenye timu ya yanga footbal club awa mchezaji nyota baada ya kuichapa timu ya rambramba Azam Fc bao mbili yeye mwenyewe uku baadae mchezeji Nyota wa Yanga Fc Simon Msuva kutundika bao la mwisho yani la tatu kwa wapinzani wao hao

mabovu story.com ndio mtandao wako kwa habari za burudani Africa na nje, Tuwe pamoja huku pia >> Instagram , Twitter Na Facebook

YANGA SPORTS CLUB KUIVAA AZAMA FC LEO TAIFA

 KIKOSI KAZI CHA YANGA FC
KIKOSI KAZI CHA AZAM FC
NGAO YA JAMII
mabovu story.com ndio mtandao wako kwa habari za burudani Africa na nje, Tuwe pamoja huku pia >> Instagram , Twitter Na Facebook

Alichosema Cristiano Ronaldo baada ya Falcao kuhamia Man United

IMG_6950.JPG
Usiku wa jana klabu ya Manchester United ilikamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao kwa mkopo.
Falcao ambaye alikuwa akiwindwa na vilabu vya Arsenal na Man City amejiunga na Man U akitokea klabu ya Monaco ambayo alijiunga nayo akitokea Atletico Madrid.
Usajili wa mchezaji umezungumzia na watu wengi mmoja wao ni mchezaji bora wa ulaya na dunia – Cristiano Ronaldo.
Akiongea jijini Madrid Ronaldo alisema: ‘Falcao ni mchezaji mzuri sana, nadhani Manchester United wamefanya jambo zuri kumsajili. Sidhani kabisa kama ni mchezaji asiyewafaa, ni mchezaji wa daraja la dunia na hivyo naamini huu usajili mzuri.”

Unaambiwa Man United wamekamilisha usajili mwingine wa huyu Muargentina.

IMG_6524.JPG
Baada ya usajili wa Ander Herrera na Luke Shaw, Manchester United wamekamilisha usajili wa mchezaji mwingine ambae ni Marcos Rojo, beki wa kiargentina aliyekuwa anakipiga kwenye klabu ya Sporting Lisbon.
Rojo ambaye alichaguliwa katika kikosi bora cha kombe la dunia, amejiunga na United kwa ada ya uhamisho wa £16 pamoja na Luis Nani kwenda Sporting kwa mkopo ambapo pia Manchester United wanaripotiwa kuhamishia nguvu zao kwa Angel di Maria wa Real Madrid.

Usajili wa Luis Suarez FC Barcelona na rekodi mpya ya gharama za usajili

20140711-165857-61137370.jpg
Baada ya uwepo wa tetesi za kuihama Liverpool kushika hatamu kwa takribani wiki 3 sasa, hatimaye leo hii Luis Suarez amejiunga rasmi na FC Barcelona akitokea Liverpool.
Usajili wa Suarez umeigharimu FC Barcelona kiasi cha £65m kwa mujibu wa mtandao wa Barcelona, na hii ni rekodi kwa Liverpool – Suarez anakuwa mchezaji aliyeuzwa kwa fedha nyingi zaidi na klabu hiyo iliyoshika nafasi ya pili kwenye EPL msimu uliopita.
Suarez ambaye alijiunga na Liverpool akitokea Ajax, pia ameweka rekodi ya kuwa mchezaji anayeshika nafasi ya nne kwa kusajiliwa kwa fedha nyingi zaidi nyuma ya Bale, Ronaldo na Neymar.
20140711-173034-63034421.jpg
Hata hivyo pamoja na usajili huo mchezaji huyo hatoweza kuitumikia Barca mpaka adhabu yake ya kufungiwa mechi 8 na kifungo cha miezi 4 kitakapoisha.

Cheki mapenzi ya shabiki huyu mwenye umri mdogo kwa mchezaji Neymar

n
Ukizungumzia taifa ambalo limetoa mastar kadhaa wa soka Duniani hutoacha kulitaja Brazil hii ni kufuatia rekodi zake kadhaa ambazo limewahi kujiwekea kwenye medali ya soka duniani leo limeingia kwa headline tena taifa hili.
Ni kuhusu mtoto mdogo amabye kwa kumtazama anaweza kuwa na umri usiozidi miaka 3,amekua ni miongoni kati ya walioumizwa na taarifa za kidaktari zinazomhusu mchezaji Neymar kuwa hatocheza mechi nyingine za Kombe la Dunia.
dogo 
Kama unakumbuka Neymar alipata majeraha baada ya kuumia kwenye mechi iliyochezwa kati ya Brazil na Colombia na katika mechi hiyo Brazil ilifanikiwa kushinda goli 2-1 na kufanikiwa kuingia nusu Fainali.
nnnnJuly 08 Brazil ambao kimsingi ndio wenyeji wa mashindano haya ya kombe la dunia itacheza na Ujeruman,mchezo utakaochezwa bila Neymar katika mechi ya Nusu Fainali.

Timu ya Algeria imerudi nyumbani kutokea kombe la dunia, hapa kuna picha 5 za jinsi walivyopokelewa

algeria 2
Kwenye kombe la dunia linaloendelea nchini Brazil, Algeria kutoka Afrika wameingia kwenye headlines zenye rekodi za kudumu kutoka kwenye mashindano haya baada ya kuwa moja ya timu mbili za Africa zilizogusa kwenye hatua nzuri kabla ya kutolewa.

Algeria 
Tayari timu hii imerejea nyumbani Afrika ambapo kiukweli imepokelewa kwa shangwe sana, na naamini hata wengine wasio Waalgeria wangeipokea timu kama hii kutokana na ilichofanya.
algeria 3 

algeria 4 

algeria 5 

Algeria 

Kuhusu kundi la wahalifu linalouza tiketi za kombe la dunia kinyume cha sheria Brazil.

ticketsJeshi la polisi nchini Brazil limesema kuwa linawashikilia watu 11 ambao wametengeza kundi linalojihusisha na uuzaji wa tiketi za kombe la dunia kinyume cha sheria.
Mtandao huo unadaiwa kuwa limejipatia fedha kinyume cha sheria kwa kuuza tiketi na tayari wamefanya uhalifu huo katika viwanja vinne vya kombe la dunia.
Baadhi ya tiketi hizo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya wadhamini wakati nyingine zikiwa zimewekwa kwa ajili ya maafisa wa timu ya Brazil.
Polisi wanaamini kuwa baadhi ya tiketi zimeuzwa kwa watalii wa kigeni.

Matokeo ya Mechi Kati ya Man City na Aston Villa Haya Hapa


Ni game full time ni Manchester City 4 magoli ambayo yamefungwa na Dzeko kwenye dakika 64′+ 72′+ Jovetic 89′ + Yaya Toure kwenye 90 +3) – 0 Aston Villa. Kwa Mtonyo huo Kwa sasa Man City Inaongoza Ligi kwa Point 83 , Liverpool Ana Point 81 ....

NGASSA AIPA YANGA BALAA LA KUKOSA UBINGWA

MSIMU uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga walikuwa mabingwa watetezi na walitumia zaidi ya Sh250 kuwasajili wachezaji watatu ambao ni kipa Juma Kaseja aliyevuna Sh40 milioni, Mrisho Ngassa aliyechota Sh30 mil na mshambuliaji Emanuel Okwi aliyeigharimu Sh180, mil.

Lakini imekumbana na balaa la aina yake imeshindwa kutetea ubingwa wake na kufanya winga wake machachari ambaye ni Ngassa kuandika rekodi ya mkosi kwa kupishana na ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa miaka mitano mfululizo.

Iko hivi; Ngassa alijiunga na Azam FC Juni 2010 kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Yanga ambayo kwa msimu huo uliomalizika haikunyakua ubingwa wa ligi. Simba walitwaa ubingwa wa msimu wa 2009/2010 tena kwa rekodi ya kutopoteza mchezo.

Mchezaji huyo aliichezea Azam kwenye msimu wa 2010/2011 na kuibuka mfungaji bora wa ligi akifunga mabao 18.

Lakini Azam ambayo ilikuwa haijawa tajiri kama ilivyo sasa, haikufanikiwa kutwaa ubingwa kwani ilimaliza nafasi ya tatu na pointi zake 44, huku Yanga wakiibuka mabingwa wa msimu huo.

Ngassa aliendelea kukipiga na Azam kwenye mwaka wake wa pili wa mkataba msimu wa 2011/2012 na licha ya kiwango chake kuwa juu kwenye msimu huo, timu yake iliambulia patupu ikimaliza ya pili katika ligi na Simba ikawa bingwa.

Bahati ilizidi kuwa mbaya kwa Ngassa baada ya kuuzwa na Azam kwenda Simba msimu wa 2012/2013 ambako nako alishindwa kuwasaidia Wekundu hao na kujikuta wakishika nafasi ya tatu huku Yanga ikiwa bingwa.

Nuksi ikaendelea katika msimu uliomalizika hivi karibuni ambapo alijiunga na Yanga, amepishana tena na ubingwa kwani sasa umeenda Azam. Ngassa amemaliza msimu akiwa na mabao 13 huku Yanga ikiwa imemaliza ya pili na pointi 56 huku Azam ikitwaa taji kwa pointi zake 62.

Mbeya City imemaliza ya tatu ikiwa na pointi 49 na Simba ya nne pointi 38

MCHEZAJI WA BARCELONA ARUSHIWA NDIZI UWANJANI..AIKOTA NA KUILA..WATU WAMPONGEZA

Barcelona star Dani Alves responded to a racist taunt in the most incredible way during a match yesterday Sunday April 27th

While playing for his team against Villareal, a spectator threw a banana at him as he tried to take a corner kick. What do you think Dani did? He casually picked up the banana, peeled it, eat the banana, threw away the peel, and then completed the kick...

This move has left many people in shock and Dani is getting a lot of praise for how he handled it.

This is not the first time the Brazilian footballer will face racism on the pitch. He complained about it last year after being taunted by monkey chants from sections of the crowd during a match at Real Madrid.

Racism in football is becoming an issue in Europe and enough is not being done to stop it. Dani is a star! Hopefully, he made the person who threw the banana feel like stupid!

SIMBA WACHUKUA MAAMUZI MAGUMU,WATEMA KIKOSI KIZIMA

UKITAKA mafanikio lazima uchukue uamuzi mgumu ambao hakuna anayeweza kufikiria kabla.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic amesema analazimika kutema wachezaji wasiopungua 11 ambao ni sawa na kikosi kizima kinachoweza kucheza mechi ya ushindani.

Lengo la Logarusic kufanya hivyo ni ili aweze kujenga upya timu ya ushindani msimu ujao.

Logarusic sasa ana uhakika wa kubaki Simba, baada ya kuhakikishiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Pope kwani awali hakuwa na uhakika wa kuendelea kubaki katika timu hiyo kutokana na mkataba wake kumalizika.

Kocha huyo atasaini mkataba wa miaka miwili baada ya ule wa miezi sita kufikia tamati.

Katika ripoti yake kwa uongozi wa timu hiyo, Logarusic amewaeleza wazi viongozi wake kuwa, ili Simba iwe na ushiriki mzuri msimu ujao wa Ligi Kuu Bara lazima nyota 11 wa timu hiyo waachwe ili wapatikane wengine watakaoisaidia timu kufikia mafanikio

DAVID MOYES KUACHISHWA KAZI MUDA WOWOTE KUANZIA LEO

Vyombo vya habari vya Uingereza, likiwemo Mail on Sunday vimeripoti kuwa David Moyes ataachishwa kazi wiki chache zijazo na kwamba anaweza kuachiswa hata leo au kesho

Wamiliki wa timu hiyo, familia ya Glazer wanadaiwa kuishiwa uvumilivu kwa kocha huyo ambaye tangu aanze kuinoa imeendelea kufanya vibaya na sasa ikiwa nafasi ya saba kwenye msimamo wa Barclays Premier League. Jana Man United ilifungwa mabao 2-0 na Everton.

Uongozi wa juu wa klabu ulikuwa umepania kumpa muda kocha huyo lakini umeona ni ngumu kuona mabadiliko kwakuwa hata wachezaji hawamwamini tena kocha wao. Ripoti hizo zinadai kuwa nafasi yake inaweza ikachukuliwa kwa muda na Ryan Giggs huku makocha wanaowaniwa kuchukua nafasi ya muda wote wakitajwa kocha wa Dortmund, Jurgen Klopp, kocha wa Uholanzi, Louis van Gaal na kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti.

YANGA NA AZAM WAZIDI KUKABANA KOO..WOTE WASHINDA LEO

Vilabu vya Azam FC na Yanga SC leo vimeendelea kukabana koo katika mbio za ubingwa wa ligi kuu Vodacom baada ya vyote viwili kupata ushindi kwenye michezo yao waliyokuwa wakicheza leo hii.
Azam FC ikiwa katika dimba la Mkwakwani ilikuwa ikicheza na Mgambo JKT na matokeo ni kwamba wamefanikiwa kushinda kwa magoli 2-0.
Magoli ya Azam yalifungwa na Brian Omony na John Bocco Adebayor.
Kwa upande wa Yanga ambao leo walikuwa wakicheza na Tanzania Prisons kutoka Mbeya katika uwanja wa taifa – matokeo ni Yanga wameshinda 5-0.
Magoli ya Yanga yalifungwa na Emmanuel Okwi, Mrisho Ngassa, Hamis Kiiza alifunga mawili na nahodha Nadir Haroub Cannavaro aliyefunga kwa penati.

YANGA YAUDUWAZA ULIMWENGU, YAVUNJA MWIKO WA WAARABU

Mabigwa wa ligi kuu Tanzania bara Young African Sports(YANGA) leo imeichapa Mabigwa wa Misri na Caf Al Ahly bao 1 - 0 nakujitengenezea nafasi nzuri
Bao la yanga lililofugwa kipindi cha pili na Nahodha Nadir Haroub "Cannavarao'' kwa mpira wa kona

HATIMAE HUYU NDIO MSHINDI WA TUSKER PROJECT FAME 6 MWAKA 2013


TB JOSHUA AITABIRIA MAKUBWA TEAM YA ARSENAL

BARCELONA YAFANYA KUFURU, YAIPIGA LEVANTE 7-0.

WHEAT CLICK THIS PHOTO