Slider[Style1]

HABARI

BONGO MOVIES

BONGO FLEVA

.

BONGO VIDEOS

Style5[ImagesOnly]

STORY ZA INSTAGRAM

Nilikua mwajiriwa katika kampuni moja maarufu jijini dare s salaam , katika kuajiriwa kwangu huko nikawa msaidizi maalumu wa bosi wa kampuni ile , basi siku moja moja nilikuwa naenda kujirusha na bosi wangu .
Ukizingatia kwamba sikuwa na mume wala mchumba na kwa kweli huyu bosi ndio alikuwa mtu wa kwanza kufanya nae tendo la ndoa , hivyo nilifurahia mhemko wake na jinsi alivyokuwa ananipenda na kunijali kila kitu nilipata na zaidi .
Alifanya yote haya bila kunificha kwamba ana mke na watoto nyumbani kwake kwahiyo wakati mwingine chochote kinaweza kutokea nijiandae kwa shuguli hiyo pevu kama mke wake akishitukia dili hilo .
Tulikuwa na uhusiano na huyu bosi kwa miezi 4 hivi mpaka siku moja katika tembea tembea mitaani nikakutana na kijana mmoja mtanashati akanieleza kwamba ananipenda na kunizimia sana yaani ameshanifia
Huyu kijana alihangaika kwa mwezi mzima mpaka siku nikaja kumkubalia akawa ndio mpenzii wangu halali sasa , nilimwamini sana nay eye aliniamini sana , miezi 3 tokea kujuana na huyu kijana aliniambia kuhusu kufanya nae tendo la ndoa .
Nilifikiria sana wakati mwingine nilitaka kulia jinsi alivyokuwa ananishika na kuniomba tendo la ndoa akiwa chumbani kwangu , alijaribu kunishika sehemu kadhaa akanivua nguo nami nilimtolea nje nilimkatalia .
Basi siku moja nikamwomba tukaangalie afya zetu , kijana wa watu alikasirika sana wiki nzima hakufika nyumbani kwangu wala kunipigia simu , kumbe alitaka tufanye tendo la ndoa bila kinga ? sasa ningejuaje kuhusu afya yake ? au ananiamini nini mimi ?
Maisha yaliendelea na mambo mengine yaliendelea tu wiki ya 3 alinipigia simu akaniomba msamaha turudiane na alikubali kwenda na mimi kupata vipimo vya afya zetu kujua kwanza kabla hatujaanza mambo mengine yoyote yale .
Basi ndio hivyo majibu yaliyoka mazuri , ndio mapenzi yetu alikuwa zaidi na penzi nilimpa bila hiyana wala aibu yoyote , yeye mwenyewe alifurahia mambo yangu na kwanza alikuwa anatoroka nyumbani kwao kuja kulala kwangu wakati mwingine mwezi mzima .
Tuliendelea kwa miezi kadha na huyu kijana huku na mimi nikiwa na bosi wangu kule kazini , basi bwana siku moja , sisi officini tulitakiwa kwenda kutoa damu hospitali ya muhimbili katika maadhimisho ya siku ya afya duniani . Watu walipimwa afya zao na mimi nilipimwa , majibu yangu yalikuwa ya kutatanisha sikuamini macho yangu wala masikio yangu , nilienda hospitali ingine napo majibu yalikuwa yale yale kwamba nimeadhirika na UKIMWI . USIKOSE KUFATILA MAKALA HAYA JUMA PILI IJAYO kumbuka makala haya yameletwa kwenue na youth africa company

About ujugu

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

WHEAT CLICK THIS PHOTO