MSANII wa filamu za Bongo, Irene Uwoya amempongeza staa mwenzake,
Blandina Chagula ‘Johari’ kwa kutumbukiza picha kwenye Instagram
ikimuonesha amevaa pete ya ndoa kwenye kidole husika. Uwoya, baada ya
kuona picha hiyo akatupia ujumbe wake akisema: Hongera mama kwa kupata
mwenzako…maaama.
Wadau mbalimbali nao walimpongeza Johari kwa hatua hiyo huku wengine wakihoji imekuwaje kimyakimya?
Maswali na pongezi hizo za wadau zilijibiwa na Johari mwenyewe ambaye
aliandika: ‘Thanx ndo maisha yanachange’ (yaani asante ndiyo maisha
yanabadilika).