The Admin is a powerful person in this world, more powerful than the president of USA. The very mention of admin sends shivers down the president. You have been warned!
Wote tumemsikia Prince Dully Sykes akiongelea kufungiwa kwa video yake
ya kabinti special na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) . Kuna sababu kuu
mbili zilizosababisha video hii kufungiwa na ya kwanza ni kitendo cha
msanii Diamond Platnumz kuvaa T-shirt iliyoandikwa neno ambalo ni tusi
. Hii ingekua kwa nchi za mbele basi ungekutwa t-shirt hii wanaifanyia
kitu kinaitwa “blurring” yaani
wanayafanya maneno yasisomeke lakini wabongo wakaona isiwe tabu na
director akaamua kuacha video irushwe ikiwa katika hali hii.Sababu ya
pili ni vazi la ufukwe yule demu alilovaa kitu ambacho dully ameona
haikua mbaya.
Mwanzoni
mwa mwaka 2014 kumeripotiwa video kadhaa za Tanzania kufungiwa huku
sababu kubwa ikiwa haijatajwa moja kwa moja,miongoni mwa watu
waliofungiwa video zao ni pamoja na Jux ‘Uzuri wako’ na video ya Snura
‘Nimevurugwa’. Millardayo.com iliwahi kwenda Basata kujua taratibu zinazopelekea
kufungiwa kwa video hizo ili kujua pia vigezo vinavyotumika kufungia
video hizo,Basata walisema wao hawahusiki na ufungiaji wa video na
kusema kazi hyo inafanywa na Shirikisho la Filamu Tanzania. February 19 Kupitia 255 ya Clouds Fm Dully sykes ambaye ni miongoni
mwa wasanii wakongwe wa muziki wa Bongo Fleva ali-amplify kuhusu
kufungiwa video yake ya Kabinti Special ambapo alisema>>’video
yangu imefungiwa wanasema kwa ajili ya maadili,wanasema sijui Diamond
amevaa fulana sijui wameandika nini na video Q2ueen sijui amevaa
swimming costume nguo ambazo hazipo kimaadili’ ‘Unajua sisi Watanzania tukifanya hivi kila siku tutakuwa hatuna
maendeleo kwa sababu ukiangalia South Africa uchumi wao unapanda kwa
ajili ya muziki,pia unachangia muziki kupanda’ ‘Nigeria pia unachangia muziki kupanda,muziki umepanda na uchumi
umepanda pia hata Kenya hapo,hata Uganda kwa ajili wao wanamuziki
wanafanya uchumi upande na nchi yao inapendeza kuona kwamba mastaa
wazuri ambao wanafanya kazi nzuri kupigwa katika nchi zote Duniani
kujulikana’ ‘Unajua msanii anapojulikana anapojulikana ametoka nchi fulani,mtu
mwingine Tanzani haijui akimuona Tunda katika MTV anajua kuna nchi
inaitwa Tanzania,kwa hiyo sisi Watanzania na serikali inabidi tuendelee
mbele kama wai wanavyoweza tunataka watuachie tuangalie maendeleo ya
sisi wanamuziki tunafika wapi’ ‘Tunabidi na sisisiku moja moja tuwe na sehemu zetu kubwa,sasa
wakitaka basi mtu akivaa swimming costume hayupo mtupu anataka video
isipigwe,hii si mara ya kwanza kwa sababu hata Nyambizi waliifungia kwa
kweli mimi walivyonikatisha tamaa ile sikutaka tena kuendelea nikasema
ngoja niangalie kitu kingine cha kufanya’
‘Kwa sababu kama nchi yangu inanikatisha tamaa nchi gani itakuja
kunisupport?kiukweli kabisa mimi naongea kama kiongozi wa wana bongo
flava Tanzania muziki wa kuimba’ ‘Serikali inabidi ituangalie sisi tunaofanya muziki ili kuipandisha
nchi yetu ili iwe kwenyue nafasi nzuri kiukweli kabisa wananchi watuache
ili tufanye kazi ili kuisaidia nchi yetu kufika mbali,sasa wanawake
wakiwa wanavaa madila kwenye nyimbo za kisasa itakuwaje’. Itazame hapa video yenyewe on AyoTV.