Wiz Khalifa hajawa Rapper wa kwanza kumsaliti mpenzi wake.Inasemekana
hii ni kawaida kwa rapper kukamatwa wakisaliti wake na wapenzi wao. Hii
list ya wasanii kumi wa Rap waliowahi kuhusishwa na usaliti.
Rapper Wiz Khalifa ameachana na Amber Rose baada ya Wiz kufumaniwa akiwa na mwanamke kitandani. Wanawake hao ni mapacha.
Kabla ya Swizz Beatz kuwa na Alicia Keys,aliwahi kutoka na msanii wa rnb Mashonda, Kwenye barua ndefu aliyoandika Mashonda miaka mitano iliyopita alisema Alicia Keys ndio aliyevunja ndoa yake na Swiz Beats.
Ja
Rule alimsaliti Karrine ‘Superhead’ kwenye kitabu alichoandika dada
huyu anasema Ja Rule alimsaliti mpaka ilifikia hatua akazoea tu. Kiabu kinaitwa Confessions Of A Video Vixen.
Kim
Porter amekuwa akitengana na kurudiana na rapper/mfanya biashara Diddy
alisema mwaka 2007 kwenye interview na Essence kuwa usaliti wa Puff
daddy na wanawake kama Sarah Chapman na kumpa ujauzito ndio sababu ya
kuvunjika kwa mahusiano yao.
Biggie na Faith Evans walifunga ndoa mwaka 1994 na baada ya furaha ya
muda mfupi, Biggie alianzisha mahusiano na msanii wake Lil Kim.
Big Boi alimsaliti mke wake Sherlita M. Patton wa miaka 11 kwenye ndoa.
Chris
Brown ni miongoni mwa wasanii wa rnb waliomsaliti Rihanna kwa muda
mrefu huku dunia ikijua kuwa mapenzi yao yana nguvu. Imefahamika kuwa
Chris alikuwa na Karrueche wakati yupo na Rihanna pia.
Nas
na Kelis walipeana talaka 2010. Sababu ya talaka yao ilikuwa usaliti wa
Nas ambao aliwahi kuhojiwa na kutubu kuwa uaminifu na usaliti ndio
umevunja ndoa yake.
Kwa
kuwa ilikuwa siri kwa rapper Fabolous ila familia ya mama wa mtoto wake
Emily B iliweka wazi kuwa mtoto wao alisalitiwa sana na rapper huyu
mpaka kupelekea kutengana.
Mwaka 2012 Mke wa Fat Joe alitaka talaka yake baada ya kuka kwenye ndoa kwa miaka 17 . Hii ni baada ya Fat Joe kuhusika kimapenzi na Ms. Dubai.
No comments: