NMB leo imefungua tawi jipya katika mji maarufu wa Kibaigwa –Dodoma.
Tawi hilo litakuwa na huduma zote za kibenki kama yalivyo matawi mengine
ya NMB nchini kote.
Tawi la Kibaigwa limefunguliwa na Naibu spika wa Bunge la Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mbunge wa Kongwa, Mh Job Ndugai.
Kufunguliwa kwa tawi la Kibaigwa kunafuatia mahitaji ya muda mrefu ya
wateja wa NMB wa eneo hilo wa kupata tawi lenye nafasi ya kutosha .Aidha
eneo hili ni karibu zaidi na wafanyabiashara wengi ambao ni wateja
wakubwa wa NMB na wananchi kwa ujumla .
Kwa kutambua pia nia ya kuendelea kuchangia huduma mbali mbali za
kijamii, benki ya NMB inatoa shilingi Milioni 10 kwa ajili ya hospitali
na shule kama shukrani za Benki kwa wananchi wa Kibaigwa kwa kuendelea
kwao kuunga mkono maendeleo ya benki.
NMB ndiyo benki inayoongoza nchini kwa kuwa na matawi mengi kwani ina
matawi zaidi ya 150, ATM Zaidi ya 500 nchi nzima pamoja na idadi ya
wateja inayofikia Milioni mbili hazina ambayo hakuna benki yenye nayo.
Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Mhe.Job Ndugai ,akiweka sahihi
kwenye kitabu cha wageni mara tu baada ya uzinduzi wa Tawi la NMB kibaigwa .
Hafla ya uzinduzi wa Tawi hilo umefanyika jana katika viwanja vya Tawi la NMB Kibaigwa Wilaya ya Kongwa mkoni Dodoma
Sehemu ya wageni Waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Mhe.Job
Ndugai akifungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la NMB Kibaigwa
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Mhe.Job
Ndugai (Kati kati)akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la NMB
Kibaigwa.
No comments: